Want create site? Find Free WordPress Themes and plugins.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) limewaondoa Waamuzi wawili kwenye orodha ya Waamuzi wa Ligi ya Mabingwa wa Mikoa(RCL) inayoendelea kwenye vituo vinne vya Geita,Singida,Rukwa na Kilimanjaro.

Waamuzi walioondolewa katika orodha hiyo ni Seleman Nonga kutoka Arusha aliyekuwa katika kituo cha Geita na Dadu Fadhil Msemo wa Kilimanjaro aliyekuwa kituo cha Singida.

Nonga ameondolewa baada ya kuonyesha kiwango hafifu cha uchezeshaji ,kushindwa kumudu mchezo,kukosa umakini,kutozingatia sheria ipasavyo kwa kipindi kikubwa cha mchezo na kupata alama ndogo katika tathmini ya Wasimamizi kwenye mchezo namba A7 kati ya Kumuyange FC dhidi ya Ambassador.

Msemo ameondolewa baada ya kuonyesha kiwango hafifu cha uchezeshaji ,kushindwa kumudu mchezo,kukosa umakini,kutozingatia sheria ipasavyo kwa kipindi kikubwa cha mchezo na kupata alama ndogo katika tathmini ya Wasimamizi kwenye mchezo namba C6 kati ya Temeke Squad dhidi ya Mtwivila City.

Waamuzi hao wawili wanatakiwa kuondoka kwenye vituo vya Geita na Singida leo Jumamosi Mei 12,2018.

TFF haitawavumilia Waamuzi watakaoendelea kuchezesha chini ya kiwango katika mashindano hayo ya RCL pamoja na mashindano mengine yote kwakuwa TFF imejielekeza katika uchezeshaji wa haki katika mashindano yake yote na TFF haitasita kuchukua hatua kali kwa yeyote atakayetaka kuharibu mashindano ya RCL.

Did you find apk for android? You can find new Free Android Games and apps.